Kauli hiyo imetolewa leo na Mhe. Rashid wakati kikao cha Arobaini cha Bunge hilo, kinachoendelea mjini Dodoma cha kujadili sura zote 15 zilizobakia za Rasimu ya Katiba Mpya, ikiwa ni mjadala wa mwisho.
"Hakuna dhambi mbaya ya kuamrisha mtu kuvunja sheria. Ninaomba sana ndugu zangu na viongozi wenzangu tutii sheria. Ndugu zangu tutulie tuendeshe nchi . Hii nchi ina bahati ya ajabu," alisema Rashid huku akisisitiza kuwa ina Rais wa ajabu ambaye anaweza kumsikiliza mtu hata ambaye anampa amri.
Mhe. Hamad aliwataka watu wasicheze na dola, huku akitolea mfano yeye na wenzake 18 waliwahi kuwekwa ndani. Hivyo aliwaasa viongozi wenzake wasicheze na Serikali, bali waitii.
Bunge hilo, ambalo linaendelea kwa mujibu wa sheria, ambapo baadhi ya wajumbe waliwataka wabunge wenzao kuendelea na kazi waliyotumwa na wananchi ya kuhakikisha Katiba inayopendekezwa inapatikana Oktoba 4,mwaka huu.
Comments
Post a Comment